Nafasi 21 za Kazi Mascons Tanzania Limited – ( Operators Mbalimbali) , Dar es Salaam – July 2026

Temporary

Website Mascons Tanzania Limited

Mascons Tanzania Limited

TANGAZO LA NAFASI ZA KAZI

JINA LA KAMPUNI: MASCONS TANZANIA LIMITED

MAHALI PA KAZI: Dar Es Salaam , Office : Ubungo Plaza, 2nd Floor

Mascons Tanzania Limited ni kampuni ya Kitanzania inayojishughulisha na shughuli za ujenzi, ukodishaji wa mitambo na mashine nzito, pamoja na usambazaji wa vifaa vya ujenzi. Kutokana na upanuzi wa shughuli zake, kampuni inakaribisha maombi kutoka kwa Watanzania wenye sifa na uzoefu kwa nafasi zifuatazo:

Nafasi Zinazohitajika

  • Backhoe Operators – Nafasi 5

  • Wheel Loader Operators – Nafasi 4

  • Self Loader Mixer Operators – Nafasi 4

  • Bulldozer Operators – Nafasi 2

  • Truck Tippers – Nafasi 6

Aina ya Ajira

Nafasi hizi ni za Casual Employment. Hata hivyo, utendaji mzuri wa kazi, nidhamu, uwajibikaji na kujituma vinaweza kumwezesha mwajiriwa kupewa ajira ya kudumu kulingana na mahitaji ya kampuni na tathmini ya utendaji wake.

Sifa za Waombaji

  • Awe na uzoefu wa kuendesha mashine au chombo husika.

  • Awe na leseni halali ya udereva inayoruhusu uendeshaji wa mashine au chombo husika.

  • Awe na uelewa wa taratibu za afya na usalama mahali pa kazi.

  • Awe na nidhamu, uaminifu, uwajibikaji na uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi.

Nyaraka za Kuambatanisha

  • Barua ya maombi.

  • Wasifu binafsi (CV).

  • Nakala za vyeti vya taaluma na mafunzo husika.

  • Nakala ya leseni halali ya udereva.

  • Majina na mawasiliano ya wadhamini wawili (Referees) wa karibu pamoja na utambulisho kutoka serikali ya mtaa.

Jinsi ya Kutuma Maombi

Waombaji watume maombi yao pamoja na nyaraka zote zinazohitajika kupitia barua pepe:

mkumilafedrick@gmail.com

Mwisho wa kutuma maombi: Tarehe 31 Julai 2026.

Kumbuka: Ni waombaji watakaochaguliwa kwa hatua ya awali pekee ndio watakaoitwa kwenye usaili. MASCONS TANZANIA LIMITED inatoa fursa sawa za ajira kwa waombaji wote wenye sifa stahiki.

DOWNLOAD PDF – MASCONS AJIRA

To apply for this job email your details to mkumilafedrick@gmail.com

Spread the love